Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kupitia Makamo wa Pili wa Rais pamoja na
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar , Mohamed
Aboud Mohamed ilipiga marufuku harakati za Uamsho na jumuiya nyengine
za kuendesha Mihaadhara ya kujadili hatma na masuala ya Muungano wakati
tume ya Kukusanya na kuratibu maoni tayari imeshazinduliwa na Rais.
Tume hii ndiyo iliyopewa madaraka ya kusimamia utaratibu wote wa kukusanya maoni pamoja na kuandaa au kuyapa Baraka makongamano, mikusanyiko na harakati za kukusanya maoni haya.
Amri hii imepelekwa kwenye vyombo vya Sheria kwa utekelezaji na na tayari tumesikia kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba alivyopiga marufuku mikusanyiko na huku Uamsho kutoa tamko rasmi kupingana na amri hii kwamba imekwenda kinyume na Katiba ya Zanzibar inayowapa haki ya uhuru wa kuabudu na kueneza dini.
Pia baada ya machafuko mwezi Mei na kutokea na uvunjifu wa amani Serikali kupitia vyombo vya ulinzi umeonekana kulifanyia kazi suala hili kisawa sawa kwa kuzuia Mihadhara na mikusanyiko ya kikundi cha uamsho.
Kipengele kinachotumika kuipa nguvu tume ni ibara 18(6) kinachoitaka tume hiyo kutoruhusu asasi, taasisi au makundi ya watu kuandaa mikutano kwa ajili ya kutoa fursa kwa wanachama wake kutoa maoni na 21(1)-(4) kinachotamka makosa mbalimbali na adhabu zake
Kinachokatazwa hapa au kinachojadiliwa kwa kadri nilivyofuatilia mwendelezo wa Mihaadhara ya Uamsho mimi sikioni au sijakitambua. Labda Wanasheria mnielimishe.
Tume imepewa hadidu rejea maalum (terms of reference) na mojawapo katika hadidu rejea hizo ni kwamba suala la Muungano lisijadiliwe wala kufikiriwa kuuvunja bali kurekebishwa na kujengwa uwe imara zaidi.
Uamsho wanachokizungumza katika Mihaadhara bila ya kumun’gunya maneno wala kutumia lugha ya istiara ni kwamba Muungano uvunjwe hawautaki kwa kutokuwa na maslahi kwa watu wa Zanzibar.
Wanachokikusanyia maoni tume ni kitu chengine ambacho kinaelekea katika kupata Katiba mpya ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania 2014 na wanachokihubiri Uamsho ni kitu chengine kabisa. Hivyo wamevunja sheria gani? Wanakatazwa kuendeleza Mihaadhara yao kwa kipengele kipi?
Uamsho wanawaelimisha waumini kwamba Muungano hauna maslahi kwayo hivyo utafutiwe njia ya kuuvunja iwe ya moja kwa moja au kwa kupitia kura ya maoni ambayo wataulizwa wananchi kama wanautaka Muungano huu au hawautaki. Sasa tukiwataka wakaombe kibali cha kuzungumza haya kutoka kwa tume ya Kukusanya maoni kwa msingi gani kwani hili halimo katika hadidu rejea za Tume.
Kwa viongozi kutoa kauli za vitisho dhidi ya wasioutaka Muungano ni kuibeza Demokrasia kwa kisingizio cha kulinda amani na utulivu wa nchi na pia kutaweza kuhatarisha mchakato mzima wa ukusanywaji wa maoni kuonekana haukuwa huru na haki kama Rais Kikwete alivyoagiza na Tume ilivyojizatiti kwamba itakuwa huru kupokea maoni yoyote.
Kama khofu ni kwamba harakati hizi zinaweza kuathiri saikolojia ya watakaotoa maoni kwa kuvutika na hoja za Uamsho hii ni khofu isiyokuwa na mashiko ya kukamatia. Uamsho hawafanyi kampeni wala kwa fikra zangu hawakuwa na haja ya kutoa tamko lolote kwani vipengele vya kisheria vinavyozungumzwa na tume haviwagusi wanauamsho kwa njia yoyote. Walipaswa kuwakabili waliokataza na kutaka ufafanuzi kwa vigezo gani na vipi shughuli zao zinakwazwa na vipengle vya tume ya Kuratibu maoni ya Katiba.
Waachieni Uamsho waendelee na shughuli zao
Tume hii ndiyo iliyopewa madaraka ya kusimamia utaratibu wote wa kukusanya maoni pamoja na kuandaa au kuyapa Baraka makongamano, mikusanyiko na harakati za kukusanya maoni haya.
Amri hii imepelekwa kwenye vyombo vya Sheria kwa utekelezaji na na tayari tumesikia kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba alivyopiga marufuku mikusanyiko na huku Uamsho kutoa tamko rasmi kupingana na amri hii kwamba imekwenda kinyume na Katiba ya Zanzibar inayowapa haki ya uhuru wa kuabudu na kueneza dini.
Pia baada ya machafuko mwezi Mei na kutokea na uvunjifu wa amani Serikali kupitia vyombo vya ulinzi umeonekana kulifanyia kazi suala hili kisawa sawa kwa kuzuia Mihadhara na mikusanyiko ya kikundi cha uamsho.
Kipengele kinachotumika kuipa nguvu tume ni ibara 18(6) kinachoitaka tume hiyo kutoruhusu asasi, taasisi au makundi ya watu kuandaa mikutano kwa ajili ya kutoa fursa kwa wanachama wake kutoa maoni na 21(1)-(4) kinachotamka makosa mbalimbali na adhabu zake
Kinachokatazwa hapa au kinachojadiliwa kwa kadri nilivyofuatilia mwendelezo wa Mihaadhara ya Uamsho mimi sikioni au sijakitambua. Labda Wanasheria mnielimishe.
Tume imepewa hadidu rejea maalum (terms of reference) na mojawapo katika hadidu rejea hizo ni kwamba suala la Muungano lisijadiliwe wala kufikiriwa kuuvunja bali kurekebishwa na kujengwa uwe imara zaidi.
Uamsho wanachokizungumza katika Mihaadhara bila ya kumun’gunya maneno wala kutumia lugha ya istiara ni kwamba Muungano uvunjwe hawautaki kwa kutokuwa na maslahi kwa watu wa Zanzibar.
Wanachokikusanyia maoni tume ni kitu chengine ambacho kinaelekea katika kupata Katiba mpya ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania 2014 na wanachokihubiri Uamsho ni kitu chengine kabisa. Hivyo wamevunja sheria gani? Wanakatazwa kuendeleza Mihaadhara yao kwa kipengele kipi?
Uamsho wanawaelimisha waumini kwamba Muungano hauna maslahi kwayo hivyo utafutiwe njia ya kuuvunja iwe ya moja kwa moja au kwa kupitia kura ya maoni ambayo wataulizwa wananchi kama wanautaka Muungano huu au hawautaki. Sasa tukiwataka wakaombe kibali cha kuzungumza haya kutoka kwa tume ya Kukusanya maoni kwa msingi gani kwani hili halimo katika hadidu rejea za Tume.
Kwa viongozi kutoa kauli za vitisho dhidi ya wasioutaka Muungano ni kuibeza Demokrasia kwa kisingizio cha kulinda amani na utulivu wa nchi na pia kutaweza kuhatarisha mchakato mzima wa ukusanywaji wa maoni kuonekana haukuwa huru na haki kama Rais Kikwete alivyoagiza na Tume ilivyojizatiti kwamba itakuwa huru kupokea maoni yoyote.
Kama khofu ni kwamba harakati hizi zinaweza kuathiri saikolojia ya watakaotoa maoni kwa kuvutika na hoja za Uamsho hii ni khofu isiyokuwa na mashiko ya kukamatia. Uamsho hawafanyi kampeni wala kwa fikra zangu hawakuwa na haja ya kutoa tamko lolote kwani vipengele vya kisheria vinavyozungumzwa na tume haviwagusi wanauamsho kwa njia yoyote. Walipaswa kuwakabili waliokataza na kutaka ufafanuzi kwa vigezo gani na vipi shughuli zao zinakwazwa na vipengle vya tume ya Kuratibu maoni ya Katiba.
Waachieni Uamsho waendelee na shughuli zao
No comments:
Post a Comment